Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea kesho kwa michezo mitano ya Mzunguko wa Nne.

Miongoni mwa michezo hiyo, itakuwa ni ile ya upinzani wa jadi kati ya JKT Ruvu itakayokaribishwa na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani wakati Mwadui itakuwa mwenyeji wa Stand United kwenye Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga.

Mbali ya michezo hiyo, pia Young Africans itakuwa mwenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, wakati Azam FC ambayo itakuwa mgeni tena kwenye Uwanja wa Sokoine ikicheza na Mbeya City na kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona Ndanda itaikaribisha Kagera Sugar ya Kagera.

Ligi hiyo itaendelea Jumapili Septemba 11, 2016 kwa Simba kuikaribisha Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, lakini uliokuwa uzikutanishe timu za African Lyon na Mbao hapo kesho umesogezwa mbele hadi Jumatatu Septemba 12, 2016. Mchezo huo utafanyika Uwanja wa Uhuru baada ya African Lyon kubadili uwanja kutoka Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Kilimanjaro Queens Yaenda Uganda
Nape Kuzuru TFF Jumamosi, Kuteta Na Malinzi