Mshike mshike wa ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu wa 2019/20 utaendelea tena leo usiku kwa michezo ya makundi manne kuchezwa katika viwanja tofauti.

Michuano hiyo inayoleta msisimko karibu duniani kote, imerejea kwa kishindo baada ya mashabiki kuanza kushuhudia vumbi likitimka usiku wa kuamkia leo kwa michezo ya makundi manne kuchezwa.

Kwa mshtuko mkubwa mabingwa watetezi Liverpool walianza vibaya kwa kufungwa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya SSC Napoli, huku mabingwa wa soka nchini Hispania FC Barcelona wakilazimisha sare ya bila kufungana dhidi ya Borussia Dortmund.

Timu ya mtanzania Mbwana Samatta KRC Genk nayo ilianza vibaya michuano hiyo kwa kufungwa mabao sita kwa mawili, huku nahodha na mshambuliaji huyo wa Taifa Stars akifunga moja ya mabao ya kufutia machozi.

Leo itakua zamu ya makundi A,B,C na D, baada ya kushuhudia michezo ya makundi E,F,G na H ikichezwa usiku wa jana.

Kundi A

Club Brugge Vs Galatasaray

Paris Saint-Germain Vs Real Madrid

Kundi B

Olympiacos Vs Tottenham Hotspur

FC Bayern Munich Vs FK Crvena Zvezda

Kundi C

Dinamo Zagreb Vs Atalanta

Shakhtar Donetsk Vs Manchester City

Kundi D

Atletico Madrid Vs Juventus

Bayer Leverkusen Vs Lokomotiv Moscow

Jordi Alba kuzikosa Granada, Villareal, Getafe
Jurgen Klopp ajitetea kwa kichapo, Ancelotti achekelea