Rapa wa Kike Mkongwe, Lil Kim amejipanga kuendeleza ushindani mkali kwenye kiwanda cha rap kwa kuangusha mixtape mpya mwezi huu.
Kupitia Twitter, Queen Bee ametangaza rasmi Machi 28 mwaka huu kuwa siku maalum atakayoachia rasmi kanda mseto yake ya ‘Lil Kim Season’.
Lil Kim amekuwa katika mtafaruku wa kiushindani na rapa mwenzake wa kike ambaye kwenye muziki anamuona kama mdogo wake, Nicki Minaj.