Tanzania imepata taarifa nzuri kutoka Marekani, ambapo usiku wa kuamkia leo Omary Tambwe maarufu kama Lil Ommy ametangazwa kuwa mshindi wa Tuzo ya Mtangazaji Bora Afrika katika Tuzo za African Entertainment Awards – USA (AEAUSA) tuzo ambayo ni ya kwanza Tanzania kuipata kwenye kipengele hicho.

Kwa mujibu wa waandaaji wa tuzo hizo zilizofanyika jijini New York nchini Marekani, Lil Ommy amefanikiwa kuwapenya washindani wake katika kipengele cha Best Host. Kadhalika, mwimbaji Nandy naye ameiwakilisha vyema Tanzania akinyakua tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kike Afrika Mashariki, Kusini na Kaskazini.

Wakali kutoka WCB nao wameibuka vinara kwenye tuzo hizo, Diamond akishinda tuzo ya Wimbo Bora wa Kushirikiana (‘Baila’, akimshirikisha Ft Miri Ben Ari) na Ray Vanny akishinda tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kiume Afrika Mashariki, Kusini na Kaskazini.

Kupitia mtandao wa Twitter, Mtangazaji huyo ambaye hivi karibuni alifanya mahojiano maalum na Dar24 kuhusu ushiriki wake kwenye tuzo hizo, amewashukuru mashabiki kwa kumpigia kura na kumfanikisha kushinda.

“Asante sana kila mmoja kwa kura zenu na sapoti yenu ya kutosha, ASANTE SANA MASHABIKI wooote kwa kura na nguvu yenu imeonekana… Love always win…. Tumeweza kuichukua tuzo ya Mtangazaji Bora wa Mwaka Afrika,” ameandika Lil Ommy.

Hata hivyo, hiyo ni tuzo ya kwanza kuinyakua kati ya Tuzo tatu alizotajwa kuwania mwaka huu akiwa Mtanzania pekee kwenye kipengele hicho.

Anasubiri majibu ya tuzo kama hiyo kwenye Tuzo za AFRIMMA zitakazofanyika Oktoba 26, 2019, Dallas nchini Marekani. Katika tuzo hizo zinazowahusisha pia wanamuziki, kwenye tasnia ya habari mbali na Lil Ommy, kutoka Tanzania pia DJ D Ommy wa Clouds Fm atakuwa anawania tuzo ya DJ Bora Afrika, tuzo aliyoinyakua mwaka 2016.

Wasanii wengi pia watahusika kwenye tuzo za AFRIMMA mwaka huu ingawa wasanii wa hip hop wamekosa nafasi hiyo.

Lil Ommy pia atawania tuzo ya Mtangazaji Bora kwenye tuzo za StarQT Awards zitakazotolewa usiku huohuo nchini Afrika Kusini.

Dar24  inawapongeza kwa kupeperusha vyema bendera ya Tanzania na tunaamini tuzo nyingine zitakazofanyika mwezi huu zitakuja pia nyumbani.

 

View this post on Instagram

 

Asante sana kila mmoja kwa kura zenu na sapoti yenu ya kutosha, ASANTE SANA MASHABIKI wooote kwa kura na nguvu yenu imeonekana… Love always win…. Tumeweza kuichukua tuzo ya Mtangazaji Bora wa Mwaka Afrika ?????? Bado zingine 2 za @starqtawards na @afrimma wiki ijayo.. Asante kwa media chache zilizosapoti, wadau mbalimbali, baadhi ya wasanii! Serikali Mhe @baba_keagan na Mhe @harrisonmwakyembe kijana wenu sijawaangusha pia Mhe DC @jokatemwegelo na wengine woooote kwa sapoti yenu. Hii ina maana kubwa sana kwangu, kwenye kazi yangu, Tasnia ya Habari na Burudani Tanzania. Asante sana team yangu @timesfmtz na Mkurugenzi @rehure_nyaulawa kwa kuniamini na kunipa nafasi toka siku ya kwanza! Asante timu yangu ya #ThePlaylist @ammygal_tz @alen_donald @nickmillz._ @djd_slash na mashabiki kwa mara nyingine tena. Bila nyinyi kwa sapoti yenu tusingefika hapa. Nyie ni Washindi pia. Tuzo hii nai dedicate kwa familia yangu, watoto wangu Rajabu na Omary ambao wanashare Birthday mwezi huu wa 10 Tarehe 23 (ingawa sio mapacha) i got two amazing boys wana share Birthday on October na Tuzo imekuja October, hii ni ishara kubwa sana. Pia na dedicate kwa vijana wote popote mlipo, usitake tamaa, usijichukulie poa, heshimu kila mtu, fanya kazi kwa bidii, sali sana, jitoe, chochote kinawezekana ukiamini ; Reposted from @aeausa (@get_regrann) – 2019 Aeaus winners. #aeausa #oneafrica @eddykenzo @stonebwoyb @ii_kaya_ises @lilommy @shattawalenima @ericomondi @dmkglobal @kalikouture_ @dance_with_judithmccarty @djkassava @mrleo237 @offlcialnandy @chetekela_official @haidymoussaofficial @mrbowofficial @afrob__ @babutale @rayvanny @matias_damasio_oficial @yobass_angola @sarkodie @michellesfoundation @mrbellomusic @diamondplatnumz @miribenari

A post shared by Omary Tambwe (@lilommy) on

Haruna Niyonzima anukia kutua Jangwani
Video: Bashungwa anadi bidhaa za ndani "tuzipe thamani ziende kimataifa''