Barua ya mwalimu Yohana Fucks imesambaa Argentina kote kwa umaarufu ikiwa ni kumwomba Lionel Messi abadili msimamo wake

Kustaafu kwa Lionel Messi kuichezea timu ya taifa ya Argentina kumeigeuza nchi hiyo juu chini siku kadhaa zilizopita, taifa lote likitetemeshwa na habari hizo baada ya Chile kuwafunga tena kwenye fainali ya Copa America.

Rais wa Argentina Mauricio Macri, Meya wa Buenos Aires Horacio Rodriguez Larreta na mungu wa soka Diego Maradona wamemuomba mshambuliaji huyo wa Barcelona kubadili mawazo yake na huenda ujumbe wote unaosambaa umekuja kupitia mwalimu wa Entre Rios Yohana Fucks.

Ombi lake limebamba kwa mamilioni ya mashabiki wa Argentina ambao wanatamani sana Messi abadili wazo lake la kustaafu soka la kimataifa.

 

Barua kamili kama inavyosomeka:

“Lionel Messi,

“Yawezekana usiisome barua hii.

Lakini naiandika, si kama shabiki wa soka lakini kama mwalimu wa Argentina, kazi ninayoipenda kama unavyopenda ya kwako.

“Ningeweza kukuandikia kuhusu vipaji vyako vya kipekee katika mchezo maarufu nchini mwetu, furaha ninayopata kuwa na fursa ya kuona kizazi cha soka na kwa bahati njema kabisa kukushuhudia ukifanya miujiza dimbani hali kadhalika jinsi unavyokonga nyoyo za mataifa yote duniani.

Kuelezea hayo nitakuwa narudia mambo. Badala yake nataka unisaidie kutatua changamoto kubwa kuliko uliyokabiliana nayo wewe. Nataka unisaidie zoezi gumu la kurekebisha tabia za watoto ambao wanakuona kama shujaa wa soka na mfano wao wa kuigwa.

“Hajalishi ni kiasi gani nina mapenzi na ubobezi katika kazi yangu, siwezi kupokea sifa nzuri sana kutoka kwa wanafunzi wangu kama ninavyokukubali. Sasa wataona mfano wao wa kuigwa ukikata tamaa.

Nakuomba usiwaridhishe watu dhaifu; wale ambao wamekasirishwa kwa kushindwa kutimiza ndoto zao maelfu ambazo walishindwa kutimiza kama wachezaji soka, wale ambao wanazungumzia mapumziko kwa sababu ni jambo rahisi kutendeka.

Unasikia hili kutoka kwa mwalimu, ambaye licha baina yetu, lakini nashughulika na tabia za Argentina za kudhani kazi ya mtu mwingine ni rahisi, kwamba kufunga magoli ni rahisi kama kujenga nyumba au mustakabali kwa ajili ya mtu.

Ni mtazamo huo unaoangusha wengi au kuzusha hoja za kijinga zikiambatana na dharau na jazba juu ya ufanisi wa wengine, kuthamini ushindi tu na kuhesabu makosa kuwa ni kushindwa, makosa hayo hayo ndiyo yanayotufanya tuwe watu na tuendelee kujifunza.

“Tafadhali usiache soka, usiwafanye wachezaji wangu waamini kwamba nchi hii inajali ushindi tu kwanza. Usiwaonyeshe kwamba hata uwe umefanikiwa kiasi gani hutaweza kuwafurahisha wengi, na usiwafanye waamini kwamba wanaishi ili kuwafurahisha wengine. Usiwape ujumbe wa makosa, licha ya kukabiliana na changamoto nyingi hadi umekuwa maarufu leo hii.

“Iwapo mtu kama wewe, mwenye familia inayokuunga mkono, ukiwa na utajiri na mashabiki wengi, huwezi, wataaminije kwamba wanaweza kukabiliana na vita hizo nyingi usiku na mchana?

“Siwaelezi ni jinsi gani Messi anacheza soka la kuvutia, lakini maelfu ya mashuti aliyopiga kufanya mazoezi ya kupeleka mpira katika kona ambayo kipa hawezi kufika.

Nawaeleza kuhusu Messi anayepata maumivu ya kuendelea kukimbiza ndoto zake; Messi ambaye kwa fedha zote alizo nazo amefanikiwa kuwasaidia watoto wenye mazingira magumu; Nawaambia kuhusu Messi aliyepevuka; baba wa familia na anayefanya kazi muhimu duniani, mzazi mwema; Messi ambaye anakosa pia penalti, makosa yetu ndiyo yanayotufanya tuwe wanadamu, na hii inadhihirisha kwamba mchezaji bora hukosea pia.

“Usikate tamaa, usitupe fulana yenye rangi za nchi yetu mbali nawe, fulana hii ya Argentina inatuwakilisha sote. Tafadhali usiwafanye wanafunzi wangu kuamini kuwa wao ni watu wa kushindwa.

“Wanafunzi wangu wanahitaji kuelewa kwamba mashujaa, wawe ni Madaktari, askari, waalimu au wacheza soka, ni wale wanaojitolea kwa ajili ya wengine hata wakijua kwamba hakuna anayewathamini au kuthamini kile wanachotoa, lakini wakiamini kwamba ushindi utakuwa ni wa wote, na kushindwa kutakuwa juu yao wenyewe. Lakini pamoja na yote hawakomi kuthubutu.

Lakini pia wana ujasairi ndani yao, wanapopambana dhidi ya kushindwa hata ulimwengu wote ukisema hatutashinda.

“Na siku moja watafurahia ushindi mkuu: Watafurahia pamoja na changamoto zote walizokabiliana nazo.

“Kila mmoja huzungumzia mpira, lakini naamini moyo wako ni thabiti.”

Video: Baada ya Mahakama kutengua matokeo ya Mbunge Nangole (Chadema), Dk. Kiruswa (CCM) amesema.....
Hans Poppe: Yanga Wameitia Aibu Nchi Yetu