Kampeni za Uchaguzi Mkuu zinaendelea ambapo jana mgombea urais kupitia Chadema anayeungwa mkono na vyama vya upinzani vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa alikuwa Muleba ambapo alifanya mkutano mkubwa wa kampeni uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi wa eneo hilo.

Lowassa alionesha kushangazwa na umati mkubwa uliojitokeza kwenye mkutano huo na kuonesha jinsi alivyofurahishwa na kuridhishwa na mahudhurio hayo aliyoyaita ‘maajabu’.

Akiwashukuru wananchi hao, Lowassa alieleza kuwa hakutegemea kama angepata mapokezi makubwa kama hayo mjini Muleba, “Sikujua kama mna mahaba makubwa kiasi hiki.”

“Tumepita maeneo mbalimbali nchini hali niliyoikuta ni kama hii hapa ya Muleba, Mungu anipe nini mie, asanteni sana,” alisikika Lowassa.

Aidha, aliwaomba kura wananchi hao akiahidi kuwaletea maendeleo kwa kasi na kupambana na umasikini uliokithiri.

Aliwasihi wananchi hao kuhakikisha wanafanya maamuzi sahihi kwa kumchagua ili wapate mabadiliko ya kweli kwenye maisha yao. Alisisitiza kuwa endapo atapewa ridhaa ya watanzania atahakikisha elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu inaanza kutekelezwa kuanzia January mwaka huu.

Serikali Ya Magufuli Kushusha Meli Tano Bahari ya Hindi
Nikki Wa Pili: Davido Alivujisha Collabo Na Joh Makini