Waziri Mkuu wa Zamani Edward Lowassa na jana aliambatana na viongozi waandamizi wa Chadema kushuhudia eneo aliloshambuliwa na kuuawa mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita, Aliphonce Mawazo.
Mwili wa Mawazo ulisafirishwa hadi mkoani Geita kutoka mkoani Mwanza baada ya kuagwa na wanachama wa Chadema, ndugu jamaa na marafiki.
Umati mkubwa wa wakazi wa Jimbo la Busanda walijitokeza kuuaga mwili wa Mawazo tayari kwa mazishi.
Marehemu mawazo aliuwa kikatili kwa kukatwa na panga na watu wasuojulikana wanaosadikika kuwa wafuasi wa chama cha siasa.