Rais Joseph Kabila amemtunuku kila mchezaji gari la kifahari la Toyota Land Cruiser Prado lenye thamani ya USD 60,000 (£40,000).
Wachezaji hao pia wamepewa nishani.
Chui hao wa Kinshasa walitwaa kombe kwa kulaza Mali 3-0 kwenye fainali na kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mara mbili.
Mwandishi wa BBC Mbelechi Msochi anasema mchezaji Heritier Luvumbu Nzinga aliyeumia kwenye michuano hiyo pia ameahidiwa kwamba atasafirishwa ng’ambo kwa matibabu.