Mtangazaji maarufu, Maimartha Jesse ameingilia kati sakata la mwimbaji Ray C kurudi katika matumizi ya dawa za kulevya licha ya kudai kuachana na dawa hizo.
Maimartha amemtaka Ray C kuweka ukweli hadharani ili asaidiwe kwani anajua kuwa anatumia dawa hizo na kwamba hata yeye yuko tayari kumsaidia aachane na matumizi ya unga.
“Ray C nakupenda saana…acha unayoyafanya Mimi najua kila kitu…nimejitahidi kukaa kimya nimeona siwezi….usimtese mama Rehema wala kaka tonny ….Mimi nakuomba acha ….nahitaji nikusaidie kupitia NGO Yangu ya #maihandhelp IG. #specialloveandcarefor#rayc Nitarudi na mrejesho soon! Nawapenda,” Maimartha ameandika Instagram.
Hivi karibuni, kumekuwa na taarifa pamoja na picha zinazoeleza kuwa Ray C amerudia enzi zake za kubwia ‘unga’ na kwamba ameondolewa kwenye orodha ya wanaopokea dozi maalum katika hospitali ya Mwananyamala.