Je unafahamu kuwa tasnia ya ubunifu wa mavazi nchini Tanzania kwa sasa unafanya vyema kulinganisha na hali ilivyokuwa huko nyuma.

Hili linaweza kuthibitishwa na hatua mbalimbali zilizofikiwa kutokana na uwekezaji mkubwa na kuibuliwa kwa tuzo mbalimbali ziinazotunukiwa kwa wabanifu wanaofanya vizuri katika Sanaa hiyo.

Sasa matamasha mbalimbali yanaandaliwa na kufanyika kila mwaka kama Tamasha la Swahili fashion linaloratibiwa na mwanamitindo mkongwe na maarufu nchini Tanzania toka India, Mustafa Hasanali ambaye anawaweka jukwaa moja wanamitindo wote kuonesha ubunifu wa mavazi yao mbele ya jopo la watu mbalimbali toka nchi tofauti tofauti na kugawa tuzo kwa wale waliofanya vyema Zaidi.

Ubunifu wa mavazi ni moja ya ngao ya utalii inayoweza kumtofautisha mtu wa taifa moja na jingine mfano kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla tuna vazi asili yaani vazi la kanga au kitenge linalofahamika karibu mataifa yote duniani kwa upekee wake.

Na tayari kazi ya ubunifu imeanza kutambulika na kupewa thamani yake inayotakiwa kama ilivyo katika mataifa ya mbali ambako tasnia hii ni moja ya tasnia pendwa na yenye kutengeneza kipato cha hali ya juu kwani wafanyakazi wa fani hii huwahudumia zaidi watu maarufu wakiwemo wasanii, walimbwende, na viongozi mbalimbali.

Utambuzi wa kazi hii nchini umeanza kuzaa matunda na kuwapa watu umaarufu mkubwa pamoja na kutengeneza ajira kwa watu wengine, kama ilivyo sasa kwa wasanii ambao wanawategemea wabunifu kujali muonekano wao na kuwa tofauti hasa wakiwa mbele ya mashabiki zao ambao hupenda kuiga au kutamani kuwa kama wao.

Hapa nchini tayari kuna jopo la watu mbalimbali wenye kipaji hiki cha ubunifu wa mavazi akiwemo, Mustafa Hasanali, Rio Paul, Hamisa Mobetto, Noel stylish, Jackline Walper, Martin Kadinda, Janeth Patrice Lumumba, Juma jux, Mama Africa sana, Speshoz  na wengine wengi ambao ni chipukizi wa tasnia hii.

Kila kilicho chema hakikosi changamoto, Tasnia hii ya ubunifu wa mavazi changamoto iliyopo ni kwamba bado watanzania hawajafunguka ipasavyo juu ya ubunifu unaofanywa na wataalamu hawa hivyo inapelekea kushindwa kutumia vyema fursa yao.

Bado kuna uzito wa kutambua umuhimu wa uwepo wa wabunifu hawa, hata hivyo utandawazi unachukua nafasi kubwa sana katika kuliweka hili sawa kwa kufungua macho ya watu na walio maarufu  kuanza kuwatumia ili kujali muonekano wao katika majukwaa na mazulia mekundu.

Aidha taaluma ya ubunifu ni moja kati ya taaluma zinazolipa endapo fursa hii ikatumiwa vizuri, hivyo basi watanzania wasipuuze uzalendo huu na kuunga mkono kile kinachofanywa na jamii hii hasa katika kutambua mchango wao katika kutengeneza maendeleo ya jamii.

Hivyo tuendelee kuwaunga mkono wanaofanya utaalamu huu na kuwatia moyo wale wanaoona wanaweza kufanya taaluma hii kwani siku hizi wanasema ”Kipaji chako, utajiri wako”.

Real Madrid wamponza Julen Lopetegui
Waamuzi wa Gor Mahia Vs Young Africans watajwa