Kama ulikuwa unaamini kuwa beki wa pembeni wa klabu ya Liverpool, Trent Alexander-Arnold ndiye mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kuliko wachezaji wote watakaoshiriki fainali za kombe la dunia mwaka huu 2018, ulikosea.

Beki huyo mwenye umri wa miaka 19 ambaye alionesha umahiri mkubwa wakati wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya na kuwa sehemu ya kuifikisha Liverpool fainali ya msimu wa 2018, ameteuliwa kuwa miongoni mwa wachezaji 23 watakaoitumikia England wakati wa fainali za kombe la dunia zitakazoanza Juni 14 nchini Urusi.

Baada ya kutangazwa kwa ikosi vya mataifa mengine yatakayoshiriki fainali za mwaka huu, imebainika Trent Alexander-Arnold ni mchezaji anaeshika nafasi ya tano kwenye orodha ya wachezaji 10 wenye umri mdogo waliotajwa kwenye timu zao za taifa, tayari kwa fainali za kombe la dunia.

Wanaomtangulia Trent Alexander-Arnold wana umri sawa wa miaka 19, lakini wmaepishana miezi, jambo ambalo linaendelea kudhihiridha kuwa beki huyo kinda wa Liverpool ni mkubwa kuliko waliomfuatia kuzaliwa kwenye orodha hiyo. Kweli kila ‘mdogo ana mdogo wake!’.

Mchezaji  Daniel Arzani wa timu ya taifa ya Australia, ambaye ni shabiki mkubwa wa Alexander-Arnold, atakuwa mchezaji mdogo zaidi kwenye fainali za kombe la dunia za mwaka huu.

Arzani mwenye umri wa miaka 19 tayari ameshaitumikia timu ya taifa ya Australia, na mchezo wake wa kwanza ulikuwa dhidi ya Jamuhuri ya Czech uliochezwa juma lililopita.

Mchezaji huyo anayecheza nafasi ya kiungo mshambuliaji kwenye klabu ya Melbourne City FC inayoshiriki ligi ya nyumbani kwao Australia (A-League), anatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwenye kikosi cha Socceroos.

Anayemfuatilia ni mshambuliaji machachari wa klabu bingwa nchini Ufaransa PSG, Kylain Mbappe, ambaye atakuwa mchezaji anayeshika nafasi ya pili kwenye orodha ya wenye umri mdogo zaidi kwenye fainali za kombe la dunia za mwaka huu.

Mbappe alizaliwa siku 15 baada ya uzawa wa Arzani.

Mshambuliaji huyo aliyeitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya UFaransa, tayari ameshajijengea umaarufu mkubwa katika soka duniani, kufuatia uwezo na umahiri wake uwanjani, lakini kilichombeba hadi kufahamika zaidi ni uhamisho wake wa mkopo kutoka AS Monaco kwenda PSG mwanzoni mwa msimu wa 2017/18 uliogharimu kiasi cha Pauni milioni 168.

Kwa msimu wa 2017/18 Mbappe aliifungia PSG mabao 21.

Makinda hawa watano watawasha moto kwenye viwanja mbalimbali vya soka nchii Urusi kuanzia kesho kutwa. Wakiwa na nafsi ya kushiriki mitanange mingi zaidi kutokana na umri wao, historia watakayoiandika kwenye fainali za mwaka huu zitakuwa na maana kubwa kwenye safari yao.

Endelea kuifuatilia Dar24, tutakujuza mengi kuhusu Kombe la Dunia, usiache kuendelea kuifuatilia Channel yetu ya YouTube ya ‘Dar24 Media’ tukusogeze Urusi.

ORODHA YA WACHEZAJI WENYE UMRI MDOGO KWENYE FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA 2018. 
MCHEZAJI UMRI TEREHE YA KUZALIWA NCHI
Image result for Daniel Arzani - australia

Daniel Arzani

19 04.01.1999 Australia
Image result for Kylian Mbappe - france

Kylian Mbappe

19 20.12.1998 Ufaransa
Related image

Achraf Hakimi

19 04.11.1998 Morocco
Image result for Francis Uzoho - Nigeria

Francis Uzoho

19 28.10.1998 Nigeria
Image result for Trent Alexander-Arnold - england

Trent Alexander-Arnold

19 07.10.1998 England
Image result for Moussa Wague - senegal

Moussa Wague

19 04.10.1998 Senegal
Image result for Jose Luis Rodriguez - panama

Jose Luis Rodriguez

19 19.06.1998 Panama
Image result for Ian Smith - costa rica

Ian Smith

20 06.03.1998 Costa Rica
Image result for Ismaila Sarr - senegal

Ismaila Sarr

20 25.02.1998 Senegal
Image result for Lee Seung-woo

Lee Seung-woo

20 06.01.1998 Korea Kusini

Urusi 2018: Nani atabeba Kombe? Tuimulike Poland
DK. Shika: Naingiza viwanda 30 nchini vya uwekezaji, 'Tutaelewana tu'