Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani amesema kuwa hakuna mwenye Mamlaka ya kutoa tamko au ufafanuzi kuhusu faru John kwa sasa zaidi ya Waziri Mkuu kwa kuwa jambo hilo liko chini ya ofisi yake. kwaajili ya uchunguzi.

Ameyasema hayo Wilayani Ngorongoro katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili wilayani humo kufuatilia changamoto za uhifadhi pamoja na utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu aliyo yatoa hivi karibuni akiwa Arusha.

“Ripoti hii ya uchunguzi ni mali ya Waziri Mkuu atakae weza kutoa ripoti hii nje kwaajili ya matumizi ya kila mmoja wetu kwa maana ya mamlaka, kwa hiyo hakuna mamlaka nyingine ya serikali yenye uhalali wa kutoa tamko au ufafanuzi wa jambo hili.”amesema Makani.

Hata hivyo, Makani amesema kuwa wanasubiri maagizo au maelekezo na mwelekeo wa sasa juu ya jambo hilo kutoka ofisi ya Waziri Mkuu.

Serikali yatoa onyo kuzungumzia Faru John
Mpango:Uchumi wetu unakua kwa kasi