Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ametoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa Kike 100 ambao wamehitimu kidato cha nne na kufaulu kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 20, 2019, Makonda amesema ameanzisha mfuko maalum wa kuwasaidia watoto wa kike waliofaulu na kusoma katika mazingira magumu kwa Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha, Makonda amesema ufadhili huo utawahusu wanafunzi wa kike waliofanya vizuri kwenye masomo ya Sayansi na kuhakikisha wanafika elimu ya juu ili waweze kulisaidia Taifa katika nyanja ya Sayansi na Teknolojia.

Makonda amebainisha makundi ya watoto watakaonufaika na mfuko huo ni pamoja na watoto wanaoishi katika mazingira magumu lakini wamefanikiwa kufaulu, watoto yatima pamoja na watoto wanaolelewa na mama wanaojihusisha na biashara ndogo ndogo.

Mfuko huo unaanza rasmi kufanya kazi mwaka huu ambapo kwa awamu ya kwanza itahusisha wanafunzi wa kike 100 waliofaulu kidato cha nne na kupata nafasi ya kuendelea kidato cha tano na sita

Tamasha kubwa la JAMAFEST latua Tanzania kwamara ya kwanza
Video: Sababu ya wanawake wa kabila hili kutoboa midomo na kuweka visahani