Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo ameendelea na ziara wilaya ya Temeke, ikiwa na lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua kwa kuzitolea majibu.

Katika ziara hiyo, Makonda amewataka  watumishi wa Halmashauri ya Temeke kufanya kazi kwa bidii  ili kupunguza matatizo mbalimbali yanayo wakabili wananchi,

Aidha,  ameongeza kuwa kufuatia kutokuwajibika kwa baadhi ya watumishi wa umma ana mpango wa kumshawishi Rais Magufuli kuwapunguza watumishi wasiofanya kazi kwa maslahi ya umma,na kusisitiza kuwa serikali inahitaji kuona kila mfanyakazi akifanya kazi kwa bidii.                                                                                                                                                                                                                                                                    Katika hatua nyingine, Makonda amewataka watumishi wa umma kujiongeza na kutotegemea bajeti ili kukamilisha miradi ya maendeleo huku akitolea mfano kuwa kwa kipindi alichokaa madarakani amepokea zaidi ya bilioni 30 nje ya bajeti, hivyo ni vyema na wao wakaiga mfano huo.

Walichosema Saut Sol kuhusu bifu la Diamond na Alikiba.
Machali aitosa ACT-Wazalendo, ahamia CCM na waraka mzito