Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA leo mchana kwa saa Afrika mashariki limepanga makundi ya michuano ya Europa League msimu wa 2018/19, katika halfa maalum iliyofanyika mjini Monaco nchini Ufaransa.

Hatua ya upangaji wa makundi ya michuano hiyo imekamilika, baada ya kutanguliwa na ile iliyofanywa jana jioni ya kupanga makundi ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Klabu ya Chelsea imeepuka kupangwa katika kundi gumu kama ilivyokua inatarajiwa na wadau wengi wa soka duniani, huku wawakilishi wengine wa England klabu ya Arsenal ikiwekwa kundi moja na Sporting CP ya Ureno.

Klabu nyingine zilizopangwa kundi moja na Arsenal ni FK Qarabag na FC Vorskla.

Chelsea (The Blues) wamepangwa katika kundi L, lenye timu za PAOK, BATE Borisov na Vidi FC.

Katika kundi hilo The Blues wanatarajia kukutana na wachezaji waliowahi kuitumikia Arsenal kama Chuba Akpom na Alex Hleb ambao wanazitumikia klabu za PAOK na BATE.

Klabu Celtic ya Scotland, imeangukia katika kundi B lenye timu za FC Salzburg, RB Leipzig pamoja na Rosenborg ambayo inatumikiwa na mshambuliaji Nicklas Bendtner, ambaye aliwahi kucheza nchini England akiwa na klabu za Arsenal, Nottingham Forest na Birmingham City.

Gwiji wa soka nchini England Steven Gerrard ambaye kwa sasa ni meneja wa klabu ya Rangers ya Scotland, atapambana na Villarreal, Rapid Vienna na Spartak Moscow katika michezo ya kundi G.

Makundi ya michuano ya Europa League kwa ujumla, baada ya kupangwa leo mchana na shirikisho la soka barani Ulaya UEFA.

KUNDI A: Bayer Leverkusen, Ludogorets, FC Zurich  na AEK Larnaca

KUNDI B: FC Salzburg, Celtic, RB Leipzig na Rosenborg

KUNDI C: Zenit St Petersburg, FC Kobenhavn, Bordeaux na Slavia Prague

KUNDI D: Anderlecht, Fenerbahce, Dinamo Zagreb  na Spartak Trnava

KUNDI E: Arsenal, Sporting Club, FK Qarabag na FC Vorskla

KUNDI F: Olympiacos, AC Milan, Real Betis na F91 Dudelange

KUNDI G: Villarreal, SK Rapid Wien, Spartak Moscow na Rangers

KUNDI H: Lazio, Marseille, Eintracht Frankfurt na Apollon Limassol

KUNDI I: Besiktas, Genk, Malmo na Sarpsborg 08 FF

KUNDI J: Sevilla, FC Krasnodar, Standard Liege na Akhisarspor

KUNDI K: Dynamo Kyiv, FC Astana, Stade Rennais na FK Jablonec

KUNDI L: Chelsea, PAOK, BATE Borisov na Vidic FC

Luis Enrique awatema Jordi Alba, Koke
Wanafunzi wa Darasa la Saba mkoa wa Simiyu wateta na RC Mtaka