Naibu Waziri wa Madini Profesa. Shukrani Manya amesema Wizara imejipanga kuhakikisha malengo ya kukusanya Bilioni 650 katika mwaka wa fedha 2021/22 yanafikiwa  kwa wakati kutokana na mikakati iliyowekwa.

Ameyasema hayo  leo  Agosti 23, 2021 Jijini Dodoma wakati wa Semina kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inayolenga kuwajengea uwezo wajumbe hao ili waweze kutekeleza jukumu la Kuisimamia sekta hiyo kikamilifu.

“Tumejipanga kuhakikisha kuwa malengo yaliyowekwaa yanafikiwa na tunavuka kwa ushauri na maoni yatakayotolewa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini tunaamini kwa pamoja tutaweza kuongeza mchango wa  sekta ya madini na kukuza zaidi mchango wake katika kukuza uchumi,” Amesema Profesa. Manya.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge  ya Nishati na Madini Dastun Kitandula, amesema kuwa wajumbe wa Kamati hiyo wamejengewa uwezo na uwelewa kuhusu sheria ya Madini ya mwaka 2017, mfumo wa utoaji leseni za uchimbaji na utafiti wa madini na ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini.

Amesema kuwa wajumbe wa Kamati hiyo  wamepata uelewa wa kutosha kuhusu ushiriki watanzania   na faida wanazopata  kutokana na sekta ya madini kusimamiwa vizuri baada ya kufanyika kwa mageuzi makubwa yanayotoa fursa kwa watanzania kunufaika na rasilimali madini.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Yahya Samamba  amesema kuwa pamoja na malengo mengine semina hiyo inalenga kuwajengea uwezo wajumbe wa Kamati hiyo ili waweze kuwasaidia katika kuelimisha wananchi katika maeneo yao na pia kuisimamia sekta hiyo .

Taliban watoa onyo kwa Marekani
Mbowe kuwatumia IGP Sirro na Ole Sabaya Kujitetea