Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi leo amefunga kozi ya waamuzi chipukizi wasiokuwa na beji za FIFA katika hoteli ya Holiday, ambapo jumla ya waamuzi 30 kutoka nchi 28 barani Afrika walihudhuria.

Akiongea wakati wa kufunga kozi hiyo Malinzi alitoa wito kwa wahitimu wajikite kwenye maadili kwa kuzingatia mafunzo waliyopata ili katika kipindi kifupi wote wapate beji za FIFA na waonekane kweye mashindano makubwa kama fainali za AFCON na mashindano ya Kombe la Dunia.

Kabla ya Hotuba ya Mgeni rasmi mwakilishi wa CAF Eddy aliishukuru TFF kwa maandalizi mazuri na usimamizi bora kwa kipindi chore cha kozi hii, na kuahidi kuleta kozi nyingine kubwa hapa nchini.

Naye mwakilishi wa FIFA Carlos Hendrique alitoa shukurani zake za dhati kwa TFF kwa kuwa tayari wakati wote kushirikiana na FIFA hali ambayo imefanyika TFF iaminike na itegemewe na FIFA kweye program mbalimbali

Kozi hiyo ya waamuzi imefanyika kwa mara ya kwanza hapa barani Afrika.

FIFA iliiteua Tanzania kuwa mwenyeji wa kozi hii kwa nchi zinazo zungumza kiingereza. Kwa upande wa nchi zinazo zungumza kifaransa kozi ya aina hii imefanyika nchini Morocco

Washiriki 30 kutoka nchi 28 barani Afrika wamehudhuria kozi hii ilivyokuwa itafundishwa na Wakufunzi wa Sita kutoka CAF na FIFA.

Tanzania Yapanda Viwango Vya Soka Duniani
TFF, NHIF Zasaini Mkataba