Mwanafamilia Mpya wa Young Africans Haji Manara amemjibu Kiungo Mshamhuliaji wa Simba SC Berbard Morrison.

Manara amejibu Morrison baada ya kuombwa kiungo huyo kutoka Ghana kuwaheshimu viongozi wake wa zamani, na kujifunza kuwa na Busara.

Manara aliyekua msemaji wa Simba SC, amerudisha majibu kwa kuandika kwenye mtandao wa Instagram.

Amemuuliza Morrison kama amewahi kumsikia akiwazungumzia viongozi wake wa zamani, na kwamba je, ni dhambi yeye kuwasifia viongozi wake wapya. Manara pia amehoji kuwa mbona alimpa Bernard Morrison sifa asizostahili?

Na pia Manara amemuuliza Bernard Morrison kuwa mbona alisimama upande wake ikiwa alikuwa anajua usajili wake haukuwa halali?

Habari kubwa kwenye magazeti leo, Septemba 1, 2021
Spika Ndugai aomba radhi