Jeshi la Marekani jana lilisema kuwa limefanya mashambulizi ya anga nchini Somalia na kufanikiwa kuwaua wapiganaji 35 wa kundi la kigaidi la Al Shabaab.

Marekani imekuwa ikifanya mashambulizi mara kadhaa dhidi ya Al Shabaab kwa lengo la kuviunga mkono vikosi vya Umoja wa Mataifa vinavyoendelea kuisaidia Serikali ya Somalia kupambana na Al Shabaab kwa miaka kadhaa sasa.

Kupitia tamko lake, Kamandi ya Marekani nchini Afrika imeeleza kuwa ilifanya mashambulizi hayo Jumapili katika eneo lililo karibu na Beledweyne mkoani Hiran nchini Somalia.

“Mashambulizi haya ya anga yalilenga wapiganaji wa Al Shabaab wenye silaha ambao walikuwa wanatawanywa kwenye maeneo mbalimbali katika vijiji,” imeeleza taarifa hiyo.

Al Shabaab wanatekeleza mashambulizi ya kigaidi kwa lengo la kuipindua Serikali ya Somalia na kusimika utawala wa kidini wenye itikadi kali.

Vikosi vya Umoja wa Mataifa vimeendelea kuiongezea nguvu Serikali dhidi ya kundi hilo, ingawa bado linaonekana kuwa na uthubutu wa kutekeleza mashambulizi katika maeneo mbalimbali.

Januari mwaka huu, Al Shabaab ilivamia nchini Kenya na kufanya shambulizi la kigaidi katika eneo la Riverside.  Makumi ya watu walipoteza maisha kutokana na shambulizi hilo.

Mourinho aeleza klabu anayotaka kufanya nayo kazi, apiga chini ofa
R Kelly afanikisha dhamana ‘kwa mbinde’