Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la soka nchini (TFF), imepitisha majina ya wagombea wafuatao kuwania uongozi katika  nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Kamati ya Uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu.

Majina hayo yamepitishwa mara baada ya kuwafanyia usaili uliofanyika Jumapili Septemba 3, mwaka huu kwenye Ukumbi wa TFF, Dar es Salaam. Uchaguzi Mkuu wa Kamati ya Uongozi wa Bodi ya Ligi utafanyika Oktoba 15, mwaka huu.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi inayotokana na kanuni za uchaguzi za TFF, majina hayo yanapaswa kutangazwa sasa.

Waliopita na majina yao kutangazwa ni Clement Sanga na Hamad Yahya wanaowania uenyekiti wakati Shani Christoms amepitishwa kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti.

Wanaowania nafasi ya ujumbe wako Hamisi Madaki na Ramadhani Mahano. Hawa wamepitishwa kuwania nafasi hizo kutoka Klabu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Pia yupo Almasi Kasongo ambaye anawania nafasi hiyo  kupitia Klabu za Ligi Daraja la Kwanza wakati Edgar Chibura anawania nafasi ya ujumbe kupitia Klabu za Ligi Daraja la Pili. James Bwire yeye hakupitishwa kwa sababu hakufika kwenye usaili.

Rais Karia aunda kamati ya tuzo
Ligi ya wanawake kuanza na ligi ndogo