Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa amemuondoa kwenye nafasi yake ya Ukurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mkoa wa Kigoma (KUWASA), Saimon Lupuga baada ya kutoridhisihwa na utendaji wake.

Mbarawa amefikia hatua hiyo baada ya malalamiko ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emmanuel Maganga kuwa mamlaka hiyo na Bonde la Mto Tanganyika pamoja na wahandisi wa maji hawatoshi kwenye nafasi zao kutokana na kufanya kazi kwa mazoea.

Kutokana na hatua hiyo Waziri Mbarawa amesema atamuagiza katibu mkuu kuandika barua ya uhamisho wa Mkurugenzi huyo kurejeshwa Dar es salaam kuanzia leo.

9

Hukumu ya Wema yasogezwa mbele
Adil Rami ajiengua Les Bleus (The Blues)