Kufuatia uamuzi wa Profesa Ibrahim Lipumba kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), watu mbalimbali wamekuwa na mtazamo tofauti huku wengi wakitaka kujua hatua hiyo imepokelewa vipi na viongozi wa Ukawa.

Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia ameelezea jinsi alivyopokea taarifa za hizo akiwa mwenyekiti mwenza wa Ukawa.

Akiongea katika mahojiano maalum na waandishi wa habari, Mbatia amesema kuwa uamuzi huo ni wa kawaida kwa kuzingatia mfumo wa vyama vingi nchini na kwamba Profesa ametumia uhuru wake kwa mujibu wa sheria.

Hii ni sehemu ya kauli ya James Mbatia:

“Ibrahim Lipumba kujiuzulu nafasi ya uenyekiti katika wa Chama Cha Wananchi CUF ni jambo la kawaida, ni mambo ya kawaida kabisa! Kwa sababu  tangu mfumo mzima wa vyama vingi vya siasa ulipoanza hapa Tanzania mwaka 1992 na vikaanza kuruhusiwa kufanya kazi kisheria, kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa, ni kwamba kila chama cha siasa ni chama shindani cha mwenzake.

“Profesa Lipumba amegombea urais mwaka 1995, 2000, 2005, ni kiongozi anaefahamika Tanzania hapa na katika siasa za vyama vingi na mchango wake mkubwa kwa taifa. Lakini hatua aliyofikia…amefikia hatua yake yeye binafsi ndani ya chama chake cha CUF. Lakini tujue kwamba kuna haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Kauli yake aliyoitoa leo ni kwamba ataendelea kuwa mwanachama wa CUF lakini amepumzika kwenye uongozi ili apatikane mwanachama mwingine aweze kukiongoza chama hicho.

“Hivi vyama vya siasa ni Taasisi, binadamu sisi tupo tunapita tu na muda wetu ukifika tunafariki, lakini Taasisi zinabaki. Mwalimu Nyerere ndiye muasisi wa TANU na CCM, mwalimu hayupo lakini CCM bado ipo. Kwa hiyo hii ni changamoto tu ya kisiasa inayotokea na hapa kwetu Tanzania mtu kutoka chama kimoja kwenda chama kingine imezoeleka”

 

 

Siku Moja Baada Ya Kuzaliwa, Mtoto Wa Diamond Apata Ubalozi
Picha: Diamond Na Zari Wapata Mtoto wa Kike