Mbunge wa Jimbo la Tandahimba kupitia tiketi ya CUF, Katani S Katani amelalamikia hatua ya serikali kulipa kiasi kidogo cha fedha kwenye vyama ushirika ambavyo viko kwenye jimbo lake linalokadiriwa kuwa zaidi ya vyama 128.

Kwa mujibu wa Mbunge Katani, mpaka sasa hakuna mkulima ambaye anamiliki magunia zaidi ya 16 ambaye ameshalipwa kutokana na utaratibu wa serikali, kulipa wenye idadi ya magunia 15.

“Kwa mfano mimi kwangu, kumefanyika uhakiki lakini fedha iliyolipwa haizidi bilioni 6, na hii fedha imelipwa kwa chama kimoja tu wakati kwangu mimi kuna vyama zaidi ya 126, kwahiyo serikali imejificha kwenye uhakiki lakini kumbe haina fedha za kutosha,” amesema Katani.

Hivi karibuni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga alisema kuwa mpaka sasa zaidi ya wakulima 130,163 wamelipwa jumla ya shilingi bilioni 133 kwenye zao la korosho.

Katika Mkoa wa Lindi tayari wakulima 41,564 wamekwishalipwa, ambapo ni kiasi cha Bilioni 42 huku katika mkoa wa Ruvuma wakulima 11,463 wamekwishalipwa kiasi cha Bilioni 10.

Aidha, Hasunga alisema kuwa katika mkoa wa Pwani Milioni 101,091,960 zimekwishalipwa kwa wakulima 81 huku akisisitiza kuwa vyama vilivyohakikiwa ni 461 na vilivyolipwa ni 451, ambapo jumla ya Kilo 40,381,798 zimenunuliwa na serikali.

Serikali iliamua kujikita kwenye ununuaji wa zao la korosho kufuatia kuibuka kwa sintofahamu baina ya wafanyabiashara na wakulima juu bei ya elekezi zao hilo hali ambayo ilipekea kusitishwa kwa minada miwili.

Manchester United uso kwa uso na Paris Saint-Germain
Fastjet yapewa notisi ya siku 28, yatakiwa ijitafakari