Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Grace Tendega, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).

Uchaguzi wa Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati 14 za Kudumu za Bunge umefanyika leo baada ya Vikao vya Kamati hizo kuanza, Jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa Kanuni za Bunge Kmati za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) lazima ziongozwe na Wabunge wa Upinzani.

Tendege alikuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chama hicho (BAWACHA), kabla ya kufukuzwa unachama na wenzake 18 Novemba 27, mwaka Jana.

Amuua mwanawe kisa kusafisha nyota
Kunenge, Mkumbo wakalia kuti kavu