Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe amekanusha vikali taarifa zinazosambazwa na watu kwenye mitandao kuwa ndiye aliyemtuma mtu aliyekamatwa na fedha mjini Dodoma.
Mtu huyo mwenye asili ya Asia anadaiwa kuwa alikuwa alipewa fedha na mmoja kati ya wagombea hao ilia toe rushwa kwa watu watakaopiga kura.
Membe amejibu kupitia akaunti yake ya Twitter:
“”Kuna taarifa za uongo zinazoenezwa kwamba kuna “Mtu wa Membe” amekamatwa na pesa Dodoma (1/2).”
"Kuna taarifa za uongo zinazoenezwa kwamba kuna "Mtu wa Membe" amekamatwa na pesa Dodoma (1/2)
— Bernard Membe (@BernardMembe) July 11, 2015
“siasa hizi ni za hovyo kwani hazitajenga Taifa letu. Naomba msihadaike na watu wanaotaka kututia doa baada ya kukosa uchafu dhidi yetu (2/2).”
siasa hizi ni za hovyo kwani hazitajenga Taifa letu. Naomba msihadaike na watu wanaotaka kututia doa baada ya kukosa uchafu dhidi yetu (2/2)
— Bernard Membe (@BernardMembe) July 11, 2015