Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba , aliamua kuwa dereva wa muda wa Lionel Messi wakati alipowasili nchini kwake kwa ajili ya kuzindua uwanja mpya.

Messi, alizindua uwanja huo unaojulikana kwa jina la ‘Port-Gentil stadium’ ambao utatumika kuandaa Michuano ya Mataifa ya Afrika mwaka 2017.

“Wakati nilipokuwa Barcelona miaka michache iliyopita, nilionana na Messi, akasema angekuja kunitembelea hapa jijini Libreville”, Bongo alisema.

“Ilikuwa ni ahadi ambayo ameitekeleza kwangu. Ni mtu wa kuheshima sana, mtu ambaye ameitimiza ahadi yake. Kalenda imekaa vizuri sana, maana ratiba yake imeenda sawa na uzinduzi wa uwanja huu”, aliongeza.

Mwaka 2012, Gabon walihodhi Michuano ya matifa ya Afrika kwa kushirikiana na Guinea ya Ikweta, ambao pia mwaka huu 2015 walihodhi peke yao.

Profesa Tibaijuka Azomewa Tena, Wananchi Wamkejeli Na Viroba
Baada Ya Kugonga Mbili, Busungu Atoa Ya Moyoni