Serikali ya Marekani na serikali ya China wamekubaliana kupitia upya makubaliano ya mikataba yao ya biashara baada ya migogoro iliyoibuka baina yao.

Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa China Xi Jinping wamefikia makubaliano ya kupitia tena mikataba yao wakiwa kwenye mkutano wa mataifa 20 yenyenguvu duniani G2O unaofanyika nchini Japani.

Licha ya kuwa hivi karibuni Rais Trump alitishia kuongeza kodi kwa bidhaa zinazoingia Marekani kutoka China kwa dola bilioni 300, amesema kuwa mazungumzo baina yake na Rais Xi yalikuwa mazuri.

Hata hivyo baada ya mkutano huo uliofanyika Osaka, Trump amethibitisha kuwa hawataongeza tena kodi kwenye bidhaa za China na wataendelea na makubaliano na China juu ya mahusiano yao ya kibiashara.

Aidha Rais Trump ametangaza kuwa kampuni za Marekani ziendelee kuuza teknolojia zao kwa kampuni ya Huawei ya China ambayo ilisitishwa kuuziwa teknolojia kutokana na sababu za kiusalama.

Ikumbukwe kuwa Marekani na China ni nchi kubwa mbili kubwa kiuchumi na wamekuwa wakiwekeana vikwazo vya kibiashara zaidi ya mwaka mmoja sasa.

Zari ampongeza Tanasha kwa kunasa ujauzito, atoa ushauri
Video: Doto Biteko aonya, 'Wizi wa madini sasa ni zilipendwa'