Aliyekuwa mwanasheria maarufu wa Serikali, Mkenya, anayeishi nchini Canada, Miguna Miguna ameapa kuuza mali zake zote nchini Kenya na pia kuacha urais wake wa Kenya iwapo kiongozi wa ODM, Raila Odinga atashinda urais.

Mwanasheria huyo ambaye uhusiano wake na Raila ulivunjika baada ya kumuapisha mnamo Januari 2018, alisema hataki waziri mkuu huyo wa zamani ashinde.

Matamshi ya Miguna yamezua mjadala moto kwenye mitandao ya kijamii miongoni mwa Wakenya. “Ikiwa Raila Odinga atakuwa rais wa Kenya, nitauza mali yangu yote huko na kuukana uraia wangu,” alisema.

Wakenya wengi walimuonya kuwa makini na matamshi yake kwani mambo yanaweza kubadilika 2022 na Raila akashinda uchaguzi wa urais.

Lynnet Swala alisema; “Lakini ulimuapisha siku za nyuma! Je, ulikataa upendeleo huo? Acha kucheza na akili zetu. Tumeamua.”

Ngere Opio alisema: “Wacha nihifadhi hii, kwa sababu mwishowe, utaondoka Kenya kwenda kwa Wakenya.”

Hata hivyo mwaka 2022, Wakenya kadhaa wamekuwa wakitoa viapo vya kile watafanya iwapo kiongozi fulani atashinda ama atashindwa katika chaguzi za urais.

Kwa mfano wakili Donald Kipkorir alisema atahamia Ureno iwapo kinara wa Orange Democratic Movement (ODM) atashindwa kwenye uchaguzi. “Chaguo langu la kisiasa la 2022: urais wa Raila Odinga au kuhamia Ureno,” alisema.

Vile vile Kipkorir na Ahmednassir Abdullahi waliamua kutumia pesa zao kubeti uchaguzi wa urais 2022. Huku Kipkorir akimfia Raila, mwenzake amekuwa mfuasi sugu wa Naibu Rais William Ruto.

Kipkorir alitangaza kuwa wamewekeza KSh 3 milioni kama pesa za kubeti wakikubaliana kuwa yule ambaye mgombeaji wake atashinda atapata pesa hizo. “Leo, tulifanya Kongamano letu la BFF Karen .. Mimi mwenyewe, @makaumutua @ahmednasirlaw. Tulijadili masuala yote kuhusu Uchaguzi wa Urais wa 2022 … naweka dau na Ahmednasir Kshs.3m ikiwa Baba au Alibaba atashinda Urais…Yeyote atakayeshindwa atalipa. mshindi. AA haiwezi kutoroka,” aliandika Kipkorir.

Uchaguzi Mkuu nchini Kenya unatarajiwa kufanyika mwezi Agosti, 2022 ili kumpata atakaechukua nafasi ya Uhuru Kenyata ambae anamaliza muda wake.

Wanandoa ambao hawajashiriki tendo la ndoa miaka 18 wakumbukwa na Mungu
Mwanamke wa miaka 51 ajifungua baada ya miaka 20 ya kuitwa Tasa