Tume ya mishahara nchini Kenya imepunguza mishahara ya watumishi wa umma wakiwemo wabunge na Rais wa nchi hiyo ili kuwza kuokoa fedha nyingi ambazo zilikuwa zikiishia kwenye kulipana mishahara.

Mwenyekiti wa Tume hiyo, Sarah Serem ametoa mpangilio huo mpya ambao amsema kuwa utaweza ku0koa jumla ya hela Ksh. 80 bilioni ambazo ni sawa (dola milioni 80 za Marekani) kila mwaka na kupunguza mishahara inayolipwa na watumishi wa umma kwa asilimia 35.

Aidha, Tume hiyo imependekeza kufuta marupurupu kwa kipimo cha usafiri wa magari kwa magavana na wabunge badala yake hilo litafidiwa kulinga na sehemu husika iliyoainishwa.

 

Hata hivyo, kwa sasa atakuwa akilipwa shilingi 1.4 milioni ambazo sawa (14,000 dola za Marekani) tofauti na awali ambapo alikuwa akilipwa shil. 1.6  milioni ambazo ni sawa na (16,500 dola za Marekani) huku panga hilo likiwaangukia wabunge.

Video: Majaliwa ategua kitendawili cha wakulima wa ufuta
Chadema yatangaza oparesheni ‘Ondoa Msaliti’