Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amepata msiba mkubwa wa kufiwa na mke wake, Linah George Mwakyembe aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Agha Khan.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Zawadi Msalla imesema kuwa shughuli za msiba huo zinafanyika nyumbani kwa Waziri huyo Kunduchi jirani na chuo cha kijeshi Jijini Dar es salaam.

Mavunde aikumbusha jamii kuhusu kudumisha utamaduni
Video: Mawaziri kitanzini, Lowassa aionya Kenya na vurugu za uchaguzi