Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo  John L. Kayombo amefanya ziara ya kushtukiza kwenye kampuni ya New Habari  Corparation iliyopo jijini Dar es salaam ambapo  miongoni mwa mambo aliyoyakuta  ni pamoja na kelele    zinazosababishwa  na mtambo wa kutengeneza magazeti katika kampuni hiyo ambazo ni hatari  kwa wafanyakazi na wananchi wanaoishi eneo hilo .

Kayombo amefanya ziara  ya kutembelea katika kampuni hiyo mara baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi na wafanyabiashara wanaoishi jirani na kampuni hiyo.
” Hili jambo sio zuri haiwezekani mashine ipige kelele kiasi hiki huku wafanyakazi wakiendelea kuzalisha magazeti,  ni  kinyume na haki za binadamu naagiza mashine hii irekebishwe mara moja ili kuondoa hii kero kwa wananchi na wafanyakazi kwa ujumla”Alisema Kayombo


Kwa upande wa wananchi wanaofanya biashara jirani na eneo hilo wamemshukuru mkurugenzi huyo na kusema kuwa kero hiyo imekuwepo kwa muda  mrefu na wametoa malalamiko yao lakini hayakufanyiwa kazi.

Waziri Makamba awataka Wafugaji na Wakulima Kuunda Kamati ya Amani
Hatari: Mwanafunzi wa shule ya msingi adai alijifunza kulawitiwa toka kwa wazazi wake