Mabingwa kihistoria barani Afrika timu ya taifa ya Misri wameicharaza Ghana mabao mawili kwa sifuri katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia za mwaka 2018 ambazo zitafanyika nchini Urusi.

Mabao ya Misri katika mchezo huo uliounguruma mjini Alexandria yalifungwa na mshambuliaiji wa klabu ya AS Roma Mohamed Salah pamoja na Abdallah Saied wa klabu ya Al Ahly.

Ushindi huo umeiwezesha Misri kukaa kileleni mwa kundi la tano katika ukanda wa bara la Afrika kwa tofauti ya point mbili wakifuatiwa na Uganda wenye point nne. Misri wamefikisha point sita.

Matokeo ya michezo mingine ya kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia ukanda wa bara la Afrika:

Libya 0 – 1 Tunisia

Guinea 1 – 2 DR Congo

Cameroon 1 – 1 Zambia

Nigeria 3 – 1 Algeria

Mali 0 – 0 Gabon

Morocco 0 – 0 Ivory Coast

South Africa 2 – 1 Senegal

Cape Verde 0 – 2 Burkina Faso

Uganda 1 – 0 Congo Brazzaville

Memphis Depay Aiangusha Luxembourg
Gareth Southgate Aipa FA Mwezi Mmoja