“Nadhani moja ya sababu kwa nini kwa miaka mingi Newcastle huwa hawapati nafasi nzuri katika msimamo wa ligi ni kwa sababu ya mtazamo huu waliojijengea. Ni kwa sababu wanachagua baadhi ya mechi za kukaza na mechi nyingine za kucheza kawaida. Huu ni mtazamo wa timu ambayo hailengi katika ushindani” – Jose Mourinho.
Baada ya kuona timu yake imezidiwa kipindi cha kwanza cha mchezo dhidi ya Newcastle, bosi huyo wa Chelsea aliamua kutoa maneno hayo makali dhidi ya Newcastle.
Katika mchezo huo Chelsea walitoka nyuma kwa magoli 2-0 na kusawazisha kupitia kwa Ramires na Willian.

Kocha Wa Dar es salaam Young Africans Apata Msiba
Familia Ya Alicia Keys Yampa Shavu Diamond Platinumz