Waziri ya Mambo ya Ndani, Dkt. Mwigulu Nchemba amemsimamisha kazi Msajili wa vyama vya kijamii, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Jumuiya za Kidini na Vyama vya Kijamii, Merlin Komba kufuatia sakata la barua iliyotumwa kwa Baraza la Maaskofu KKKT na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Dkt. Nchemba amesema kuwa Serikali imeanza kufanya uchunguzi na endapo watabaini aliyetengeneza barua hiyo kwa taasisi hizo za kidini watamchukulia hatua kali za kisheria.

Amesema uamuzi wa kumsimamisha kazi Komba kupisha uchunguzi unatokana na taharuki iliyosababishwa na barua hiyo isiyokuwa na baraka za Serikali.

Aidha, amevishangaa vyama vya siasa ambavyo vilianza kutoa matamko na misimamo hata kabla Serikali haijatoa kauli yake.

Jana, Uongozi wa Bunge ulimzuia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kujibu swali la mbunge wa upinzani kuhusu kilichoandikwa kwenye barua iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii, ililolipa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kufuta waraka iliotuoa wakati wa Pasaka.

Spika Ndugai alifikia uamuzi huo kwakuwa swali hilo liligusa suala la dini ambalo amewahi kuzia lisijadiliwe ndani ya Nyumba hiyo ya wawakilishi wa wananchi.

Barcelona yalipa fadhila kwa Eric Abidal
Jonny Evans ajiunga na Leicester City