Serikali wametakiwa kuipokea kwa mikono miwili sheria ya makosa ya ya mtandao kwa kuwa inalenga katika kuwafaidisha zaidi kwa kuwalinda dhidi ya wizi wa mtandaoni, udhalilishaji na kuingiliwa faragha.

Hayo yameelezwa na waziri wa Mawasiliano, Sayansi Na Teknolojia, Profesa Makame Mbawara alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.

Profesa Mbawara alitoa mfano wa watu wanatumia simu na mitandao kufanya utapeli unaowapa hasara kubwa wananchi, na pia picha zisizofaa zinazoumiza hisia za watu wanaoguswa moja kwa moja na tukio hilo.

“Picha ambazo saa nyingine kumetokea accident pahala, watu wameumia vibaya lakini watu wanazipeleka kwenye mitandao,” alisema. “Leo tu mtu anaamka anatuma ujumbe kila mahala, picha za matukio ya kutisha yanayosababisha wananchi waweze kuchanganyikiwa,” aliongeza.

Aidha, Profesa Mbawara aliwataka wananchi kutodanganywa kuwa sheria hiyo imetungwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Alifafanua kuwa sio kweli kuwa anaepokea ujumbe wa kichochezi na zisizofaa ataingia hatiani bali yule aliyetuma ndiye anayetakiwa kukutana na mkono wa sheria. Alisema mtumiwaji wa meseji akifuta bila kusambaza hataingia hatiani.

Ingawa kanuni za sheria hiyo bado hazijatungwa, Profesa Mbawara alieleza kuwa serikali imejipanga vizuri katika kutekeleza sheria hiyo inayoanza rasmi leo, Septemba 1.

“Serikali imejiridhisha baada ya kufanya maandalizi yote muhimu ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa umma na kujenga uelewa kwa watekelezaji wa sheria hizi,” alisema.

Amewataka wananchi  kutumia vizuri mitandao ya kijamii kwa manufaa ya kila mmoja kwa maendeleo ya taifa.

Mbokani Kucheza Soka England 2015-16
Man Utd Wampata Mbadala Wa Wayne Rooney