Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amesema kuwa mtoto wake mwenyewe alipata maambukizi ya virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa covid -19 lakini amepona kwa kujifukiza.

Amebainisha hayo leo alipokuwa anatoa salamu zake baada ya kushiriki ibada ya jumapili katika ushirika wa KKKT Chato mkoani Geita na kubanisha kuwa hofu juu ya corona ni hatari zaidi kuliko ugonjwa wenyewe.

Katika kuthibitisha hilo ameamua kutolea mfano jinsi corona ilivyoingia kwenye familia yake na kusema kuwa mtoto wake mwenyewe alipata ugonjwa huo hivyo anaufahamu.

“Mimi ninapozungumza hapa nina mtoto wangu alipata corona, mtoto wa kuzaa mimi, amejifungia kwenye chumba akaanza kujitibu amejifukizia akanywa malimao na tangawizi amepona mzima sasa anapiga push up” Amesema Rais Magufuli.

Amesema wananchi wanapaswa kufahamu kuwa ugonjwa huu utasambaa lakini baadaye utaisha, na wananchi hawanabudi kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga.

Corona Tanzania: Vyuo, Michezo kufunguliwa, Utalii bila karantini
Balozi wa China - Israel akutwa amefariki nyumbani kwake