Hatimaye, Mungu amejibu maombi ya mwanamitindo wa kimataifa Mtanzania, Happiness Millen Magese kwa kumpatia mtoto wa kiume baada ya kilio cha miaka mingi akipigana vita kali na ugonjwa wa endometriosis.

Mrembo huyo ambaye alishinda taji la Miss Tanzania mwaka 2001 ame-share na dunia habari njema na furaha yake kupitia mtandao wa Instagram akimshukuru Mungu kwa kumpa baraka aliyokuwa akimuomba kwa muda mrefu.

Mrembo huyo ameandika ujumbe kwa mwanae akimtaka kuwa baraka, matumaini na muujiza kwa mamilioni ya wanawake duniani wanaotamani kupata watoto lakini wameshindwa kutokana na kuwa na ugonjwa huo.

“Ukalete matumaini, imani na miujiza kwa mamilioni ya wanawake duniani wanaotamani kubeba watoto wao kama nilivyokuwa nikitamani kukubeba wewe. Ukue na kuibadili dunia kwa ajili ya wengine. Ukamuamini Mungu na kumiliki miujiza yake,” ameandika mrembo huyo.

“Kwa kadiri ambavyo maisha yanaweza kuwa magumu, ujifunze kuwa mvumilivu, ufanye kazi kwa bidii na ukijua kuwa kila kitu wakati wote hutokea kwa sababu na kila binadamu ana njia yake na Mungu ana mpango kwao,” aliongeza.

Millen Magese aliweka wazi kuwa mtoto huyo anampa jina la baba yake mzazi, akieleza kuwa hatimaye amempata baba yake.

May you bring Hope ,faith and Miracles to millions women out there who wishes to hold their children just the way I wished to hold you. May you grow to change the world and be there for others . May you believe in God and own his miracles . As much as life can be tough ,may you learn to be patient, work hard and knowing that ,everything always happens for a reason and every human being has their own path and plans from God for them. Don’t ever loose hope . And no matter what happens in your life remember,you have our God Almighty and I will be here always . Father I thank you for making me A Woman and Finally A mother . Father I thank you for bringing my dad back What a gift .jina Lako Lihimidiwe ??? I love you my Son ❤️ And to you godmother @funminewyork . I believed you had a good heart you have been with me for 13 years but Gosh what you have done through out my pregnancy journey is unexplainable. God bless you sis I can’t say more . ????? Prince Kairo Michael Magese was born Time :6 .58 am Weight :9 pounds 2 oz Date :July 13 th 2017 . You’re my Victorious just like the meaning of your name “Kairo” Glory to God . Dansaki . Asante Mungu Many thanks to Dr Seckin @endofound , Dr Lobo,Dr Gyamfi and the whole team from Columbia Doctors . Many thanks to all my friends and family oooh you guys tried @theojinika @lebogangm @samanthajansen @jimi_mugul .Special thanks to all Endometriosis groups World wide for all you do . We will raise awareness till we find Cure ??.And to you all my supporters thank you , Don’t stop supporting us. I believe A cure for Endometriosis is almost here . Support Us???? To Everyone don’t you ever forget ,If you knew who walked beside you, at all times, on the path that u have chose, you could never experience fear or doubt again,Have Faith ??Stand on Your Faith ??Change Your Story ??You Can Do It?? Millen Magese ? #PrinceKairo?

A post shared by Millen Magese (@ladivamillen) on


Kwa miaka mingi, Millen Magese amekuwa akisumbuliwa na endometriosis, na aliamua kuanzisha harakati za kuwasaidia wanawake wanaosumbuliwa na ugonjwa huo duniani kote hususan Afrika.

Amekuwa mstari wa mbele kutoa msaada kwa mashirika yanayojihusisha na kutoa huduma za kujitolea kwa umma hususan matatizo ya uzazi kwa wanawake.

Ujumbe wa Magese utaifikia dunia nzima kwa urahisi kwani ni mrembo aliye chini ya makampuni makubwa ya mitindo kama Ford Models la New York Marekani na Ice Mode Management la Afrika Kusini, na amekuwa akipewa nafasi na vyombo vya habari vya kimataifa kama CNN.

Dar24 inampongeza Millen Magese kwa kupata mtoto wa kiume. Mungu ambariki.

Mawakili wa Trump watofautiana na msemaji wao, aamua kujiuzuru
LIVE: Ziara ya Rais Magufuli mkoani Kigoma