Kampeni za uchaguzi wa ubunge zikiwa bado zinaendelea katika majimbo ya Kinondoni, Siha na kata 10, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi amevikumbusha vyama 12 vinavyoshiriki uchaguzi utakaofanyika februari 17, 2018 kuendesha uchaguzi huo bila kuvunja sheria za nchi.

”Natambua kuwa baadhi ya vyama vyenu vinashiriki katika chaguzi ndogo za ubunge na udiwani zinazoendelea katika majimbo na kata. Hivyo natumia fursa hii pia kuvipongeza vyama vyote vinavyoshiriki katika uchaguzi” amesema Jaji Mutungi.

Aidha ameviasa vyama vinavyoshiriki uchaguzi kuheshimu na kufuata sheria ya vyama vya siasa, sheria ya gharama za uchaguzi na kanuni zake, kwa kuepuka vitendo vya fujo na lugha za matusi na uchochezi .

Pia Jaji Mutungi ametoa wito kwa wanachama wa chama chochote cha siasa au kinachoshiriki uchaguzi kutoa taarifa katika mamlaka husika kuliko kujichukulia sheria mkononi.

Dkt. Kalemani akagua miradi ya uzalishaji Umeme Katavi
Watoa huduma za usingizi wahitajika