Kamati ya waamuzi nchini imemteua mwamuzi Jonesia Rukyaa kupuliza kipenga katika pambano la watani wa jadi, Simba na Yanga siku ya Jumamosi.

Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Jonesia kukabidhiwa jukumu la kuwa mwamuzi wa kati katika pambano hilo. Jonesia aliweka rekodi ya kuwa mwamuzi wa kwanza mwanamke kuchezesha mechi ya watani wa jadi nchini alipochezesha pambano la Nani Mtani Jembe mwaka juzi.

Jonesia Rukyaa 01

Jonesia atasidiwa na Josephat Bulali kutoka Tanga, Samwel Mpenzu (Arusha). Wakati mwamuzi wa akiba  ni Elly Sasii  kutoka Dar huku Kamisaa wa mchezo huo akiwa Khalid Bitebo kutoka Mwanza.

 

Tanzia: Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa afariki
Mfungaji Bora Wa Ligi Ya Afrika Kusini Afariki Dunia