Mlinzi wa kushoto wa timu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania  Mwinyi Haji Ngwali (Bagawai) anajivunia kucheza kombe la mapinduzi kwa miaka mitatu mfululizo kwa timu tatu tofauti.

“Ukweli ni jambo zuri kwenye maisha ya Soka kucheza kombe kama hili miaka mitatu mfululizo kwa timu tatu tofauti, najivunia na pia ninafuraha sana, kwanza nipo nyumbani Zanzibar, pili kombe hili naliheshimu kwani limenipa umaarufu mkubwa mimi binafsi, na pia nimejisikia furaha sana nilipoiyona familia yangu wamekuja hapa Amaan kuniangalia Babaangu mzazi na Kaka Makame umewaona wamekuja kunipa sapoti, ukweli nina furaha KISANDU mpaka sina tena cha kusema”. Alisema Mwinyi.

Mwinyi Haji alianza kucheza kombe hilo mwaka 2014 (Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar) akiichezea timu ya Chuoni na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa mchezaji bora kwenye mashindano hayo.

Mwaka 2015 akaitumikia timu ya Mabaharia ya KMKM na mwaka huu anatoa huduma yake katika timu yake mpya ya Yanga pia ameweka rikodi ya kucheza kombe hilo mara tatu mfululizo akihudumu timu tatu tofauti kila mwaka.

Marcello Lippi Awaponda Guardiola, Mourinho Amkubali Ancelotti
Ronaldo De Lima Amkubali Messi Kuliko Wajina Lake