Mbunge wa Jimbo la Mtama kwa tiketi ya CCM, Nape Nnauye, amepata ajali ya gari leo asubuhi akiwa safarini kuelekea wilayani Liwale kushiriki kikao cha kamati kuu ya siasa ya mkoa wa Lindi.

Imeelezwa kuwa hakuna madhara makubwa yaliyotokea kwa waliokuwa ndani na nje ya gari hilo, ambapo Nape Nnauye alikuwa njiani kwenda kuungana na ziara ya Katibu mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally anayezuru wilaya ya Liwale.

 

LIVE: Waziri Mkuu akishiriki kukinasua kivuko cha MV Nyerere Ukerewe mkoani Mwanza
Maharamia wateka wahudumu 12 wa meli