Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameitaka timu ya soka ya Tanzania Bara Kilimanjaro Stars kususia mechi na Libya, kuonyesha kutokubaliana na vitendo vya biashara ya utumwa inayoendelea Libya.

Ameyasema hayo, katika ukurasa wake wa twitter, ambapo amesema kuwa ni vyema timu ya Kilimanjaro Stars ikasusia mchezo huo.

“Nashauri Tanzania isiingie uwanjani kucheza na Libya. SADC iagize nchi zake zote zirudishe mabalozi wake kutoka Libya, ili kuonyesha kuchukizwa na Biashara ya Utumwa,”ameandika Zitto

Aidha, Zitto amewataka Watanzania wachukue hatua kuonyesha kuchukizwa na kupinga vitendo hivyo vya ukatili na ukiukwaji wa haki za binadamu, vinavyoendelea nchini Libya.

Airtel Tanzania yatoa msaada kwa Jeshi la Zimamoto
Songas yaipa serikali zaidi ya bilioni 11