Mchezo namba 152 wa mzunguko wa 19 wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Ndanda FC ya Mtwara na Young Africans umepangiwa tarehe ya kuchezwa.

Bodi ya Ligi imetaja tarehe hiyo baada ya awali mchezo tajwa kutokuwa umepangiwa tarehe kwa mujibu wa ratiba ya Ligi Kuu.

Mchezo huo sasa utachezwa Jumatano Februari 28, 2018 katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona uliopo mkoani Mtwara.

Timu zote tayari zimejulishwa kuhusu tarehe ya kuchezwa mchezo huo.

Video: Waziri Dkt. Kigwangalla awajibu Polisi
Paul Put abwaga manyanga Kenya, FKF wasaka mbadala wake