Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa mashine za kuandisha kwa njia za kielekroniki zilizokamatwa katika kiwanda cha MM Steel, Mwenge, jijini Dar es Salaam sio mashine za BVR kama ilivyodaiwa awali.

Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima amesema kuwa baada ya kuzifanyia uchunguzi mashine hizo, wamebaini kuwa mashine hizo ni ‘feki’ na hazifanani na mashine zilizotumiwa na Tume hiyo.

“Hakuna ukweli wowote kwamba zile ni mashine za BVR na tumebaini ni feki. Tena ni sawa na zile zinazotumika kwenye ofisi mbalimbali kuandikisha wafanyakazi wake. Hao waliosema ni mashine za kuandikisha wapiga kura hawako sahihi, sio kweli,” alisema Kailima.

Kailima alieleza kuwa walifanya uchunguzi wa mashine hizo wakiwa pamoja na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani vinavyounda Ukawa kwa kuwa wao ndio waliiopeleka malalamiko kuhusu uwepo wa mashine hizo.

Mashine hizo zilimatwa juzi baada ya kuhisiwa kuwa na uhusiano na mashine za BVR kwa kutokana na mfanano wake na njia zilizokuwa zinatumika kuwaandikisha wafanyakazi kiwandani hapo. Mashine hizo tayari zilikuwa zimeandikisha wafanyakazi 100.

Meneja Mawasiliano wa MM Steel alieleza kuwa mashine hizo zilitumika kwa lengo la kuandikisha wafanyakazi hao ili kupata taarifa zao kwa lengo la kupunguza wizi uliokuwa ukifanywa na baadhi ya wafanyakazi na kutokomea.

Kuhusu Kuahirishwa Kwa Uchaguzi Wa Ubunge Arusha Mjini Na Mazingira Ya Kifo Cha Mgombea
Lowassa Awamulika ‘Mama Na Mtoto’, amjibu Magufuli