Mama watoto wa Diamond Platinumz, Zari Hassan amethibitisha na kutangaza kifo cha mama yake mzazi ambaye siku chache zilizopita taarifa zilizagaa mitandaoni kuwa amelazwa hospitalini na anapumulia mashine.

Zari Hassan kupitia mtandao wake wa instagram amepost ujumbe mzito wenye majonzi makubwa kumuaga marehemu mama yake na kumtakia pumziko la milele na amani.

”It’s with deep sorrow that my family and I announce the death of our lovely mother who passed on this morning. May her soul rest in peace, May Allah forgive you your sins and grant you Jana.
You will forever be loved our Old Sun, us as your kids were given the best from God as our mother. We appreciate all you did for us. We will forever cherish you Mama.Sleep well?” ameandika Zarithebosslady.

Hata hivyo mwaka huu umekuwa pigo kubwa sana kwa mwanamke Zari Hassan kwani mnamo May 5, alimpoteza baba wa watoto wake watatu Ivon Don ambaye aliumwa kwa muda mfupi na kufariki dunia.

Mungu amtie nguvu Zari Hassan katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Mungu ailaze roho ya marehemu huyo mahali pema peponi na apumzike kwa amani.

 

Mbunge wa Jimbo la Temeke aswekwa rupango
Lowassa kitanzini tena, atinga kwa DCI kuhojiwa