Hatimaye Rais wa Marekani, Barack Obama amezungumzia taarifa zilizokuwa zimesambaa kwenye mitandao kuwa mkewe, Michelle ana mpango wa kugombea Urais siku za usoni.
Kupitia mahojiano aliyofanya na Rolling Stone, Obama amesema kuwa mkewe hana mpango wa kuingia kwenye siasa.
“Michelle hatagombea kamwe,” alisema Obama. Nafahamu ni mtu mwenye kipaji ninachokifahamu,” aliongeza.
Endapo Michelle angewania nafasi ya urais, angekuwa amefuata nyayo za Hillary Clinton aliyewania nafasi ya urais mwaka huu akiwa mke wa Rais mstaafu wa Marekani, Bill Clinton.