Madiwani wa Halmashauri za Wilaya ya Kilwa  na Ruangwa Mkoani Lindi Wameanza Utekelezaji wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID) kwa Kupatiwa Mafunzo ya Siku 4 na Kuratibiwa na Tamisemi

Kuanza kwa Hatua Hiyo kunafuatia kumalizika kwa Mafunzo kwa Watendaji wa Halmshauri 6 Za Mkoa wa Lindi juu ya Namna ya Kushiriki na Kutekeleza Mradi huo Utakaotekelezwa kwa Kipindi cha Miaka 5 Ijayo

Akifungua Mafunzo hayo,Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi amezitaka Halmashauri Hizo Kufuatilia kwa Umakini Mafunzo yanayotolewa na wakufunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa Hombolo ili Kupata Uelewa Juu ya Uendeshaji wa Halmashauri

‘’ Madiwani ni kiungo muhimu baina ya serikali na watendaji wa serikali madiwani Musipokuwa Vizuri Mtaburuzwa na Watendaji hususan katika Utendaji na Utekelezaji wa Miradi hasa Ikiwa Diwani Una Tabia ya Kuomba omba na Kukopa kwa Mkurugenzi au Mkuu wa Idara Lazima Mjipime Nyie Ndio wamiliki wa Halmashauri au hamjijui?’’Alimalizia Zambi

picha 1Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi Akilakiwa na Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini,Suleiman Bungara(BWEGE)Mara Baada ya kuwasili katika Ukumbi wa MM Hotel Mjini Lindi kwa Ajili ya Ufunguzi wa Mafunzo Elekezi kwa Madiwani Wa Halmashauri za Kilwa na Ruangwa ili Kuelewa Jinsi ya Kutekeleza Mfumo ya PS 3.

PICHA 2Mkuu wa Mkoa wa Lindi Akitoa Hotuba yake ya Ufunguzi ambapo Pia Aliwataka Madiwani Kuacha Siasa katika Kutekeleza Maendeleo ya Halmashauri zao,Kulia ni Mkurugenzi wa Shughuli za Mikoa Mradi wa Ps,Bw Conrad Mbuya.

PICHA 3Baadhi ya madiwani na watendaji wa halmashauri za Kilwa na Ruangwa Mkoani Lindi wakifuatilia jambo katika semina Elekezi ya Kujenga Uelewa kwa Halmashauri kupitia Mradi kuimarisha Uwezo wa Kutoa Huduma kwa Jamii Chini ya Utekelezaji wa Mradi wa PS3 Unaofadhiliwa na USAID.

PICHA 4Afisa Mshauri wa Masuala ya Utawala Bora PS3, Nazar Sola akitoa Elimu kwa Madiwani juu ya Utekelezaji wa Mifumo ya Utendaji na Utoaji Huduma.

PICHA 5Bw Joel Shimba,Mshauri wa Utawala Bora PS3(Kushoto )Wakielekezana jambo na bw Victor Msoma,Mshauri wa Fedha PS3(Kulia)Kuhusiana na Mafunzo ya madiwani wa Kilwa na Ruangwa Huku Bi Nseya Kipilyango,Mshauri wa Mifumo ya Tehama wa PS 3(Katikati)Akifuatilia kwa Umakini.

PICHA 6Lukelo Mhenga Mhasibu Msaidizi(kushoto) pamoja na Fina Maziku wote wa PS 3 wakifuatilia mada katika mafunzoa Hayo ambapo Halmashauri za Wilaya zao za Kilwa na Ruangwa zikiwa ni Halmashauri za Awali kati ya 6 za Mkoa Huo Zilizoanza utekelezaji wa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya sekta za umma(PS3) katika sekta za afya, elimu na kilimo.

PICHA 7Madiwani wa Ruangwa Pamoja Na Mwandishi wa Vikao Vya Baraza la Madiwani Ruangwa,Bahati kasabano (Kulia)wakifuatilia mafunzo hayo.

PICHA 8Madiwani na Watendaji wa Halmashauri Pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri Hizo ambao nao  wanashiriki mafunzo hayo ya Siku 4 yanayofanyika Mjini Lindi.

Video: Waziri Mwakyembe hafurahishwi na mambo haya ya upinzani.
Ronald Koeman Kuhamia Goodson Park