Rais John Magufuli, leo amemtembelea Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad katika Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam.
Maalim Seif alilazwa katika hospitali ya Hindul Mandal baada ya hali yake kiafya kubadilika kutokana na uchovu aliopata kwa kusafiri kutoka India alikoenda kupata matibabu hadi Zanzibar, na baadae kuingia jijini Dar es Salaam.