Meneja kutoka nchini Italia, Roberto Di Matteo ametambulishwa rasmi mbele ya vyombo vya habari, baada ya kukamilisha mpango wa kusaini mkataba wa kuwa mkuu wa benchi la ufundi la klabu ya Aston Villa, ambayo msimu ujao itashiriki ligi daraja la kwanza huko England.
Wakati wa utambulisho huo, Di Mateo  mwenye umri wa miaka 46, alionekana ni mwenye furaha sanjari na mmilili wa Aston Villa, Tony Xia ambaye ni mmiliki mpya.
Utambulisho wa Di Mateo amefanyika katika uwanja wa Villa Park ambao unatumiwa na klabu ya Aston Villa ambayo maskani yake makuu yapo mjini Birmingham.
Di Mateo  akiwa na mmilili wa Aston Villa, Tony Xia
 Dr Xia,  Di Matteo na mtendaji mkuu wa Aston Villa Keith Wyness.
Di Matteo akionekana mwenye furaha.