Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amemteua Dk. Musa Mgwatu kuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA).

Kabla ya Uteuzi huo Dk. Mgwatu alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika Hodhi la Rasilimali za Reli (RAHCO) ambapo kwasasa ameteuliwa kuchukua nafasi ya Mhandisi Marcellin Magesa ambaye amepangiwa majukumu mengine Wizarani..

Akitoa taarifa hiyo Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Joseph Nyamhanga amesema , Profesa Mbarawa pia amemteua, Masanja Kadogosa ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRL) Kukaimu nafasi ya Mtendaji Mkuu wa RAHCO.

Idadi ya wasomi Kilimanjaro yapungua, wanafunzi 230 ni wajawazito
Yemi Alade amtamani Ali Kiba